Kundi la Mafikizolo la Afrika Kusini limejigamba baada ya kushinda tuzo nane katika tuzo za Afrika Kusini zinazojulikana kama South Africa Music Awards (SAMA).
Kundi hilo linaundwa na Nhlanhla Nciza na Theo Kgosinkwe ambalo liko nchini Nigeria hivi sasa, limefanya mahojiano leo na The Beat 99.9 ya Lagos.
“Ni kama tulichukua tuzo zote kwenye SAMA.” Alijigamba Nhalanhla. “Tulichukua tuzo 8 usiku ule.”
Wasanii hao walieleza pia maana ya jina la kundi lao kuwa ni ‘New Comer’, kwa tafsiri ya Kiswahili isiyo rasmi tunaweza kusema ni watu wanaoanza katika sehemu fulani au wageni.
Mafikizolo walitambulisha rasmi wimbo wao ‘Tchelete’ waliomshirikisha Davido. Wimbo huo umetayarishwa na wasanii watu wa Afrika Kusini ambao ni Uhuru, Oskido na Shizza.
Wameeleza kuwa ‘Tchelete’ maana yake ni good life/maisha bora.
Usikilize hapa:
No comments:
Post a Comment